
Na Gasto Kwirini wa Jeshi la Polisi Arusha
Ikiwa
ni siku ya tatu tangu kuanza kwa operesheni ya ukaguzi wa magari Mkoani
Arusha, leo tarehe 11.07.2019 muda wa asubuhi imebainika baadhi ya
Wamiliki, Madereva na Makondakta wameanza kuitikia wito wa kutozidisha
abiria katika mabasi yao na kufuata sheria bila kushurutishwa.
Operesheni
hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa
Arusha Mrakibu wa Polisi (SP)Joseph Bukombe imeanza kuonyesha matokeo
chanya baada ya ukaguzi kufanyika katika Mabasi yanayofanya safari zake
kati ya Arusha na Kiteto, ambapo hayakuzidisha abiria kama ilivyozoeleka
kwa mabasi mengi yanayopita njia hiyo.
Akitolea
mfano Basi la Kampuni ya Mtei Express, Mkuu huyo wa Usalama barabarani
ameipongeza kampuni hiyo, dereva pamoja na Kondakta kwa kuitikia wito
wake alioutoa kwa wamiliki, madereva na Makondakta kwa kuhakikisha
wanafuata Sheria za usalama barabarani, ambapo mabasi mengi yalikua
yanajaza Abiria kuliko uwezo wa gari.
"Kwanza
nimpongeze mmiliki wa Mabasi ya Mtei, nadhani Elimu ya Utii wa Sheria
bila shuruti ameanza kuifanyia kazi, leo tumekuja mpaka Custom na
tumekuta basi lake likiwa levo siti, namuomba aendelee kufanya ivo ivo
hatagombana na Jeshi la Polisi lakini akizidisha abiria tunageuka hadi
kituoni tunaanza moja na Abiria wote waliozidi atawatafutia usafiri
mwingine". Alisema RTO wakati akizungumza na Abiria wa Basi hilo..
Sambamba
na hilo amefanya ukaguzi wa malori yanayobeba mchanga katika maeneo
mbalimbali hasa katika barabara ya Arusha - Simanjiro/Kiteto na kubaini
ubovu mkubwa katika malori hayo hasa uchakavu wa matairi.
Amesema
zoezi la ukaguzi wa Malori hayo amelianza rasmi na atafanya kazi usiku
na mchana ili kuhakikisha malori yote mabovu hayapiti barabarani. Pia
wamiliki wa magari hayo kuyafanyia matengenezo hasa kuyafunga tairi mpya
kwani mengi tairi zimeisha.
"Zoezi
la kukagua malori ya mchanga linaanza upya, na leo tumewafuata uku
wanakochukua mchanga lengo ni kuhakikisha kwamba malori hayo yanarudi
katika hali nzuri kama zoezi tulilolifanya mwaka ambapo tuliagiza
wayatengeneze na walifanya ivyo, sasa naona wamejisahau". Alisisitiza
RTO.
Aidha amesisitiza
kwamba endapo watayafanyia matengenezo magari yao, madereva wao
watafanya kazi kwa uhuru bila usumbufu wakiwa barabarani.
Naye
Wakala wa Mabasi ya Mtei Express Bwana amepongeza Operesheni,
amesisitiza iwe endelevu kwani itasaidia kuwakumbusha Wamiliki kukagua
magari yao kila mara pamoja na kuwadhibiti madereva, na Makondakta
wanaovunja sheria.
Theophil
Fredrick Makala, Dereva na Mkazi wa Kwamrombo, amelishukuru Jeshi la
polisi kwa ukaguzi wanaondelea kuufanya kwani inasaidia magari yao kuwa
salama kwani inapelekea wamiliki wa magari kuyajali hasa kuyatengeneza
kila mara na pia ukaguzi huo unawafanya wao kuwa na nidhamu kwa kufuata
sheria za usalama barabarani.
Jumla
ya Malori matano yamekamatwa na kufikishwa katika Kituo Kikuu cha
Polisi Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa ajili ya kufanyiwa Ukaguzi
zaidi ili yaweze kuadhibiwa kwa mujibu wa Sheria.
1.
Picha No. 1. Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu wa
Polisi (SP) Joseph Bukombe akishuka katika basi baada ya kulifanyia
ukaguzi ambao unaendelea Mkoani Arusha
2.
Picha No. 2. Vijana wakisukuma noja kati ya lori bovu ambalo
limekamatwa na Jeshi la Polisi katika Operesheni inayoendelea ya ukaguzi
wa magari Mkoani Arusha.
3.
Picha No. 3. Moja kati ya tairi ya Lori ambayo inaonekana ikiwa katika
hali ya uchakavu ambapo limekamatwa katika Operesheni ya ukaguzi wa
Magari inayoendelea Mkoani Arusha
4.
Picha No. 4. Baadhi ya malori yaliyokamatwa kwa ubovu katika Operesheni
ya Ukaguzi wa Magari inayoendelea kufanyika mkoani Arusha.
0 Comments